Bukobawadau

SIMULIZI ;UNFORTUNATE LOVE SEHEMU YA 1.

katika maisha yangu ya kimapenzi nilishwahi kutoka na kufanya mapenzi na wanaume wanne na nikadanganywa, nikaumizwa na kukosa raha, nilikuwa natumiwa kama chombo starehe pasipo kujijua mimi mwenyewe ila ni mwanaume mmoja tu ambaye alinionjesha utamu wa mapenzi na kunipenda, kunijali na katika mikono yake nilihisi kama ni mwanamke wakipekee sana kuzidi wengine…..Ni kwasababu gani niliwahi kufanya mapenzi na wanaume wanne na ni mwanaume gani ndiye aliyenipa na kunionjesha utamu wa mapenzi??? Sikiliza kwa makini nikuelezee yalionitokea mpaka ikawa hivyo.

SEHEMU YA 1.

Naitwa sarah james, mimi ni mtoto wa pili wakike kutoka kwenye familia ya bwana James ambaye ni baba yangu mzazi na Anna amabaye ni mama yangu mzazi, Kwenye familia yetu tupo wanne; mimi; baba yangu; mama yangu na dada yangu aitwaye suzy. Mimi pamoja na familia yetu tunaishi kinondoni, morocco na familia yetu ni tabaka la kati kwa maana sio maskini sana wala sio matajiri sana. Maisha yangu yalilemea sana katika mapenzi na kupitia huko niliyaona mengi na kujifunza vingi na pia katika maisha yangu ya kimapenzi nilishwahi kutoka na kufanya mapenzi na wanaume wanne na nikadanganywa, nikaumizwa na kukosa raha, nilikuwa natumiwa kama chombo starehe pasipo kujijua mimi mwenyewe ila ni mwanaume moja tu ambaye alinionjesha utamu wa mapenzi na kunipenda, kunijali na katika mikono yake nilihisi kama ni mwanamke wakipekee sana kuzidi wengine. Najua watu wengi mnaweza sema kwamba haya yote nilijitakia mwenyewe au kufanya kwa makusudi ila sio kama hivyo mnavyofikiria ninyi. Ni kwasababu gani niliwahi kufanya mapenzi na wanaume wanne na ni mwanaume gani ndiye aliyenipa na kunionjesha utamu wa mapenzi??? Sikiliza kwa makini nikuelezee yalionitokea mpaka ikawa hivyo.

Nilimaliza shule ya msingi mwaka 1993 na mwaka 1994 nikaanza elimu ya sekondari, nikajiunga Na shule ya mzizima secondary school iliyopo hapa Tanzania, nilianza masomo yangu katika shule hiyo nikiwa sina mtu ninayemfahamu wala kumjua na pia mwanzoni mwa masomo yangu nilikuwa bado sina rafiki ninayemzoea. Ilipita kama wiki moja hivi na pia nakumbuka hiyo siku ilikuwa jumamosi ya wiki na pia ilikuwa sio siku nzuri kwangu hasa mda ule wa jioni ambapo nilichelewa kufika katika eneo tuliokuwa tunagaiwa chakula basi nilipofika katika eneo lile nikakuta washamaliza kugawa chakula na mimi sikupata hata kijiko kimoja cha mlo. Basi nikatoka katika eneo lile na kwenda nje kidogo huku nikiwaza nitakula nini kwa usiku ule, punde si punde akatokea msichana mmoja ambaye nasoma naye kwenye darasa moja na alikuwa anafahamika kwa jina la Rachel.

Rachel aliponiona katika dibwi la mawazo aliniita “Sarah vipi, Kunatatizo gani?” name sikusita kumwambia na nikamuelezea tatizo langu ya kuwa nimekosa chakula basi Rachel akaniambia “usijali twende tukale wote ili usije ukalala na njaa”, basi nikamshukuru sana na tangia siku ile mimi na Rachel tulikuwa marafiki wakaribu sana. Siku zikapita na sisi pia tukiendelea na masomo yetu ya kidato cha kwanza tukiwa tunaizoea shule yetu ya Mzizima secondary school na pia uhusiano baina ya walimu na wanafunzi ulikuwa mzuri.
Siku moja mimi na Rachel tuliamua kwenda kutembelea darasa lililokuwa jirani yetu amabalo ni ‘kidato cha kwanza b’ na lengo letu la kwenda kwenye darasa hilo lilikuwa ni kuwasalimu marafiki zetu wengine, basi tulipoingia tu katika hilo darasa macho yangu yakagongana na macho ya mvulana mmoja aliyekuwa akiketi mwishoni mwa darasa, tuliangaliana kwa kama sekunde kumi mpaka Rachel akanishitua nakuniita “ Sarah! Sarah! Sarah! Vipi mbona umeganda kwani umemwona nani?” name nikamficha nikamwaambia “hamna, basi tu.” Kisha tukaenda kuketi mbele ya darasa walipoketi marafiki zetu ambao ni ‘Leila’ na ‘Sharifa’. Tukiendelea kuongea nao basi yule mvulana alitoka kule alipoketi nakuja pale tulipoketi sisi akisemezana nasi “ mambo zenu wadada” nasi tukamjibu na kumwambia “ poa tu”, aliendelea kuongea na Sharifa akimwambia “ hawa wageni wa leo umewatoa wapi” sharifa hakusita kumwambia nakusema “ hawa ni marafiki zetu wa darasa la kidato cha kwanza A, huyu kulia kwangu anaitwa Sarah na huyu mbele yangu anaitwa Rachel” naye akajibu “ nashukuru kuwafahamu nami naitwa Eric”, huku akininyooshea mkono nami nikaupokea na tukatizamana huku wote tukitoa tabasamu zuri basi marafiki zangu Rachel, Leila na Sharifa waliguna nakusema “ mmh aya yetu macho na masikio.” Baada ya muda mfupi tukaondoka katika lile darasa na kurejea darasani kwetu na kumalizia vipindi vyetu vya mchana.

Sharifa na Eric walikuwa marifki wazuri sana na wanaelewana vizuri sana, basi Eric alikuwa anataka kujua mengi juu yangu na hakusita kumwambia sharifa kwasababu ni rafiki wake ambaye anamuamini katika kila jambo pia Sharifa nae alikuwa akimdokeza Eric baadhi ya vitu kuhusu mimi kama tabia yangu na jinsi nilivyo kwa ujumla na Eric alikuwa akifurahi kusikia vingi vizuri kuhusu mimi basi Sharifa akamuuliza swali gumu sana Eric akisema “ Eric, kunakitu unanificha na bado hutaki kuniambia na sijui kwa nini?” Eric akamjibu, “ Sharifa embu kuwa muwazi ni kitu gani wataka kujua kutoka kwangu?” Sharifa akaendela kunena “ ni kuhusu Sarah, je unampenda au…?” Eric akainamisha kichwa chini na kukaa kimya kwakama sekunde kumi na tano na kasha kumwangalia Sharifa na kusema “ siku ile ya kwanza kuonana na Sarah niliguswa sana moyoni na pia nawea kusema nipo kama nimeonjeshwa sukari na kuikuta sukari kuwa tamu na yenye kunivutia. Sharifa ninaamini ninampenda Sarah kutoka moyoni mwangu.” Basi Sarah alifurahi kusikia hivyo kwakuwa si mwenye wivu akamwambia Eric “hongera zako kijana umeshaona ua lako zuri likichanua kwenye bustani sasa bado weye kulichuma” Eric akacheka akisema “Sharifa unamambo weye”

N: B

Falling in love with someone is not a crime/sin and when you firstly fall in love with someone you can’t stop being nervous because you will be thinking of ways to express to that person what you really feel for him or her but you just don’t know what is the exact right way to do it? - Rodrique Romio’s quotation

Source;rommyzcity.blogspot
Next Post Previous Post
Bukobawadau