Bukobawadau

HARUSI YA NATASHA YA KUKUMBUKWA.

ILIKUWA ni siku ya kipekee katika historia ya tasnia ya filamu pale mwanadada na mdau mkubwa katika tasnia ya filamu Susan Lewisy ‘Natasha’ alipofunga pingu za maisha na Mr. Alex Humba katika kanisa la Mt. Joseph tarehe 27/7/ 2013 saa sita mchana tofauti na harusi nyingine ambazo zimezoeleka zinazofanyika kila uchwao.

Monalisa akiwa na mdogo wake.Baada ya harusi hiyo ya kipekee kufungwa na kuhudhuriwa na waheshimiwa mbalimbali wakiwepo wasanii, maharusi walitoka na kuelekea Hotelini kwa ajili ya upigaji wa picha sambamba na kupumzika kabla ya kwenda ukumbini kwa ajili ya kusherekea ukumbi wa kisasa wa Magereza uliopo Ukonga.

Mr & Alex walipendeza kupita maelezo kwani kitu kilichowafanya wapendeze zaidi ilikuwa ni tabasamu lao sambamba na mavazi waliyovaa kwa siku hiyo maalumu kwao na kwa marafiki zao waliofika kwa kumsupport Natasha kama rafiki kipenzi wa jamii nzima ya tasnia ya filamu Swahiliwood, walipendeza sana na kuandika Hitoria ya maisha mapya.
.

Sherehe hizo zilipambwa na msafara wa mastaa wanaokuja kwa kasi katika tasnia ya filamu Bongo Jalila na Jamira wakiwa na Sonia binti Tyson wakiongozwa na mwigizaji nyota na maarufu asiyechuja Afrika Yvonne Cherryl aka Monalisa ambaye pamoja na umakini alipendeza kweli kweli na kuwa ni pambo la Harusi ya Natasha na kuwaziba midomo wale wote waliokuwa wakikejeli ndoa hiyo.
Uongozi wa FC unatoa pongezi kwa maharusi wetu Mr & Mrs Alex kwa kuungana na kuwa mwili mmoja na si wawili tena, Mungu abariki maisha yao ya ndoa Takatifu iliyofungwa na Mungu. Ameni. Natasha ni kiungo muhimu sana katika tasnia ya filamu Swahiliwood kwa mawasiliano na mwongozo pia kwa wasanii wote.
Next Post Previous Post
Bukobawadau