Bukobawadau

CHECK KINACHO ENDELEA MSIBANI KWA MAREHEMU HASSAN MUNJURI (HANS)NYUMBANI KWAKE KILIMAHEWA KASHAI BK MAPEMA YA LEO

Mdau Amani Mwarabu mfanyakazi wa Kampuni ya Sigara mwenzake na Marehemu Hassan Munjuri maarufu kama(Hans )akionyesha jeraha la risasi, baada ya kujeruhiwa na mtu asiyejulikana na mtu huyo kumuua Marehemu Hans tukio lililotokea usiku wa tarehe 7 Dec.2013 na kupelekea hali ya wasiwasi kutanda mjini hapa.
 Ndg Amani akijaribu kutoa maelezo mbele ya mwanalibeneke wetu juu ya mkasa,kama utavyo ona katikati ya habari hii hapo chini
Marehemu Hassan Munjuri ameacha Mjane,watoto wawili pichani na kichanga kimoja.
Picha ya Marehemu Hassani Munjuri (Hans)wakati wa uhai wake,Marehemu alikuwa mfanyakazi wa kampuni y TCC.Jeshi la Polisi bado linaendeleana uchunguzi wa kifo hicho.
Mwenyezi mungu ailaze roho yake mahala pema peponi Amen!
Waombolezaji waliofika msibani hapo.
Mzee Abdallah King, Mzee Kitenge na Mjomba Ismail(kipara)
 Super Self Mkude kushoto akiomboleza msiba wa mwanachama mwenzake wa 'Pamoja Group' na mwana bukoba veteran, yupo Mzee Yakubu na Mzee Salum Kapara( Mawingo)
Matukio yote ya bukobawadau yanaatikana papo hapo kupitia ukurasa wetu wa facebook , unachotakiwa kufanya ni kufungua link hii na kutupia like tu, gonga https://www.facebook.com/Bukobawadau?ref=hl
Mdau  Reuben Sunday rafiki mkubwa wa Marehemu Hans, akichukua matukio ya kumbukumbu.
 Sehemu ya wadau wanachama na wachezaji wa Bukoba Veteran
Taswira ndani nyumbani kwa marehemu Hassan Munjuri.
 Hivi ndivyo hali ilivyokuwa msibani hapa kwa mchana wa leo jumapili dec 8,2013
 Bi Vannesa pichani kushoto, Mgeni Idrisa kwa mbali anaonekana Dada Lilian.
 Kila mtu akihoji kujua kinacho na kilochoweza kutokea/endelea, ni mwendo wa kuulizana tu!!
Camera yetu ikicheck na wadau wakimiminika msibani.

Baadhi ya waombolezaji waliofika msibani nyumbani kwa marehemu Hassani Munjuri(Hans).
Sehemu ya wanadada ambao ni wanachama wa 'Pamoja Group' wakiwa na nyuso za huzuni kufuatia msiba huu.
Sehemu ya waombolezaji

Ndugu mwinyi akionyesha picha ya Marehemu Hans.
 Wadau wakimsikiliza majeruhi wa tukio hili, Ndg Amani maarufu kwa jina la mwarabu akisimulia juu ya mkasa wa tukio zima la mauaji akisema yeye na mfanyakazi mwenyake wa TCC marehemu (Hans) Hassan Munjuri walifika katika hotel ya BukobaCup zamani Yaasila iliyopo pembezoni mwa fukwe za ziwa victoria ikiwa ni muda mchache baada ya kumalizika kwa sherehe ya family day iliyokuwa imeandaliwa na Ofisi yao.
Walichokifanya yeye na mwenzake baada ya Sherehe hiyo walielekea makwao wakiwa wameongozana na familia /wake zao.Baada ya kufika nyumbani ikabidi warudi tena Hotelini hapo kwa lengo la kulipia vinywaji na huduma mbalimbali walizozipata hotelini hapo.
 Ndg Amani anaendelea kusema kwamba mara baada ya utaratibu wa kulipia gharama hizo wakaamua kuondoka,ile tu wanafika sehemu ya maegesho wakakuta Gari lao limezuiwa ndipo wakahitaji msaada kutoka kwa mhusika wa gari lililowazuia/ aliye block ili waweze kuondoka.
Kwa subira tofauti kufika tu kwa jamaa huyo  kukatokea  majibishano,vijembe na kuparurana kwa maneno ya hapa na pale, na kushikana mashati
Ndipo Mdau Amani akajaribu kumtuliza huyo jamaa ambaye hadi sasa hajajulikana ni nani,anasema kitendo cha kumsogelea tu huyo jamaa akatoa silaha na kumshambulia begani na kuanguka chini.
Jamaa huyo akaendeleza shumbulizi la risasi lililomlenga sehemu ya kichwa Marehemu Hans  Hassan Munjuri nakupelea mauti yake, kisha mhusika akatokomea na Gari lake dogo aina ya Saloon.
 NOTE:Maelezo ya mkasa huu ni kwa mjibu wa Majeruhi wa tukio hili, Ndg Amani.(mwarabu|)
 Wadau wakiendelea kufika msibani hapo
Waombolezaji wakishughulikia mpango wa mapishi.
 Upande wa kina mama hivi ndivyo walivyojipanga
 Hope wa Makoko akiwajibika.
 Hekaheka za maandalizi ya msosi
Mdau Temmy Felix Mnyama.
Mdau Optaty Henry , Mbaraka na mwenzao wakibadilishana mawazo.
Yupo pia Mdau Fedelis Kaiza.
 Marafiki wa karibu wa marehemu Hans ikiwa ndio wanafika kuwafariji wafiwa.
 Mdau Bi Salome mama Chui na London akiteta jambo na Dada Lilian Peter Mwise.
 Kijana Chichi Salum.
Sadick athmani akibonga na wenzake.
Wakiwa katika hili na hili kama ilivyo kawaida.
Ndg Patrick Pombe na Mdau Said Bunduki.
Kushoto ni Abdulrazak Majid, Sadi Idd, Mwishi na Paul.
BUKOBAWADAU BLOG TUNATOA POLE KWA FAMILIA , NDUGU JAMAA WA MAREHEMU, TUNATOA POLE KWA WAFANYAKAZI WENZAKE WA TCC NA KWA WANACHAMA NA WACHEZAJI WA BUKOBA VETERAN
Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu Hans Hassan Munjuri Mahali pema Amen!!





Next Post Previous Post
Bukobawadau