Bukobawadau

MTIKILA:KUNA CHADEMA MBILI - 'CHADEMA CHUMBANI' NA 'CHADEMA SEBULENI'

Mchungaji Christopher MTIKILA azidi kupiga msumali wa MOTO katika JENEZA la Chadema mashumbulizi yake yamuelekea Edwin MTEI

"Amemtuhumu mmoja wa wanzilishi na m/kiti wa kwanza wa chadema Edwin MTEI, akidai kuwa ni muasisi wa dhana ya UKABILA na UKANDA katika chama hicho huku m/kiti wa sasa Freeman MBOWE na Katibu wake SLAA wakidaiwa kuboresha mfumo huo KISASA zaidi kwa kuweka NAKSH NAKSH"

Hata kinacho wafukuza Zitto na wenzake ktk Chadema ni matokeo ya kuota mizizi kwa mfumo wa UKABILA na UKANDA ambao hauruhusu mwanachama yoyote kuhoji mapato na matumizi ndai ya chama"

WATANZANIA waelewe Chadema si chama cha siasa na VIONGOZI wake si wanasiasa wa kweli, kwani hawana MAONO wala MALENGO ya kuwakomboa watanzania

KWA UJUMLA NI GENGE LA WALAJI TU!!!

Ndani ya chadema kuna kundi linaitwa "BIG EIGHT " ambalo linaudwa na wazee wa KICHAGA na kiongozi wao mkuu ni Edwin MTEI akisaidiwa na akina Mariale na Ndessamburo,

Hawa ndio wenye chadema yao ambapo moja ya MAJUKUMU yao ni kulinda maslahi ya kichaga ndani ya chama,Kuna Chadema mbili kuna chadema ya CHUMBANI na Chadema ya SEBULENI"

Source gazeti la Umma Tanzania 4/12/2013
Next Post Previous Post
Bukobawadau