Bukobawadau

MWIGULU AMLIPUA MBOWE BUNGENI NI KUHUSU KUTUMIA VIBAYA MADARAKA YAKE!!

Mh. Mwigulu nchemba madelu, mbunge wa iramba magharibi katika mwongozo alioomba kwa spika wa bunge asubuhi hii amemlipua kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni FREEMAN MBOWE kwamba ametumia madaraka yake vibaya na kuharibu image na heshima ya bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania kwa kukatisha ziara ya kikazi ya mbunge wa viti maalumu chadema mkoa wa arusha joyce mukya ambaye alisafiri kwa kazi za kibunge kwenda Dominica Republic,lakini akiwa new york, MUKYA alipokea simu ya MBOWE kuwa akatize safari yake na kwenda Dubai aungane naye kwa "kazi maalumu' . 
MWIGULU ameomba mwongozo kuwa uongozi wa bunge umchukulie hatua mh mbowe kama mtu binafsi badala ya hivi sasa ambapo taasisi nzima ya bunge inachorwa vibaya mbele za jamii ambapo Habari zilizopo kwenye top page za magazeti ya leo yamelichafua bunge zima kumbe mhusika mkuu ni mbowe ambaye ameelezwa kuwa alimwamuru joyce mukya arudi kutoka safarini badala yake aende dubai kwa kazi maalumu wakati tayari alishapokea posho ya bunge kwa safari ya kikazi. 

Aidha mwigulu ameomba mwongozo wa kufanyika uchunguzi wa mahesabu kuhusu posho zilizotolewa na bunge/serikali halafu mhusika hakwenda kwenye safari iliyokusudiwa.badala yake mbunge ameenda kuvinjari na hawara

Next Post Previous Post
Bukobawadau