Bukobawadau

YALIYOJILI MKUTANO WA BALOZI KAGASHEKI JIMBONI KWAKE LEO JAN 23,2014

Majira ya saa kumi alasiri, Ndege maalumu ikiwa inawasili  katika uwanja wa ndege mjini hapa.
Mh. Balozi Khamis Juma Sued Kagasheki akiwapungia mikoni wananchi waliojitokeza kumpokea.
 Kagasheki na wananchi hayo ni maneno yanayo someka katika vazi la mwanachama.
 Wadau katika mapokezi hayo.
 Burudani ya ngoma mwanzo mwisho.
 Jamco na Super Jeanifer Murungi Badru Kichwabuta wakicheck na Camera yetu

Wananchi wakimpokea Mh. Balozi Kagasheki.
'The boldgard 'Jumanne Bingwa.
 Hakika ni furaha kubwa kwa mamia ya wananchi waliojitokeza katika Uwanja wa ndege.
Wadau wakipambana katika kumuongoza Balozi Kagasheki kuweza kupata njia.
Ilikuwa vigumu kupata njia kwa namna watu walivyo mlaki Mbunge wao maarufu 'swahiba'
 Watu full kwechoncha na swahiba wao.
Uwanjani kuna wakati watu walipotezana.
 Mzee Kambuga akifanya 'kuwhatsaap' hapa ndipo tulipo fikia na utandawazi
 Wadau ndugu wa familia ya Kagasheki.
 Sehemu ya waratibu  mipango ya yote tunayo yashuhudia leo
 Kijana Mkushini na wadau wengine, muhimu kwako mdau pitia order post kupata hotuba kamili.
 Kijana Avit Kato pichani kulia na Mohammed Moha Nyundo.
 Mama na mwana wakibanjuka.
 Ni taswira mbalimbali  juu ya yaliyojili katika mapokezi na mkutano wa Mh. Kagasheki.
 Mdau Mr Mpoma, wakitambo sana huyu.
Pitia hotuba Older post upate matukio zaidi na hotuba kamili ya Mh. Kagasheki
 Mh. Balozi Khamis Kagasheck akicheck muda kabla ya kusaini kitabu cha Wageni.
Baada ya kusaini kitabu cha wageni anasalimiana na Haji Abbakari Galiatano na Haji Sadick Galiatano.
Balozi Kagasheki anasalimiana na Komredi Mzee Luangisa, Kitu Muhimu kutoka kwetu mdau msomaji utapa kusikiliza audio juu ya alichokisema Mzee Luangisa kupitia hapa hapa Bukobawadau Blog.
Nje ya Uwanja wa Ndege, bango linasomeka hivyo.
 Mwanzo wa maandamano makubwa ya kumpokea Mh. Mbunge Balozi Khamis Kagasheki
 Jengo la Ofisi chama cha mapinduzi mkoa Kagera
 Naamm ni kidedea mbele ya ofisi za CCM .
Maeneo ya Polisi, barabara ya Samuel Luangisa.
 Pwaa pwa pwa pwa Eee kidedea pwa pwa pwa pwa ee kidedea!!
Mguu kwa Mguu, hatua kwa hatua,kidea hadi maeneo ya Soko kuu Mjini Bukoba.
Katikati ya Viunga vya Mji wa bukoba,watu wanaimba, wanaruka, ni mwendo wa miduara na rusha roho.
Mtiti wa watu walio hudhuria katika mkutano huo.
 Mwalimu Joyce akifuatilia kile kinacho endelea.
Mwanzo wa ufunguzi wa Mkutano huu ameongea Diwani Ibra Manyema kama mwenyeji.
 Makamu meya wa Manispaa ya Mji wa Bukoba , Mzee Ngalinda  akimkaribisha Mh. Mbunge Kagasheki jimboni mwake, sambamba na kutoa utambulisho kwa madiwani wote waliohudhuria.
 Mahudhurio makubwa mno ni zaida ya darasani !!
 Utaratibu upo hivi watu wamekaa, wametulia pasipo shaka wakisubilia makamuzi ya Mh. Mbunge Balozi Khamis Kasibante Sued wa Kagasheki.
 Kushoto ni Mh. Ibrahim Maburouk , Diwani kata ya Bilele (CUF)
 Hamimu Mahmudu Omary, katibu mwenezi wa CCM Mkoa.
 Mh. Samuel Ntambala Luangisa, Diwani kata ya Kitendaguro akitoa neno kidogo.
 Taswira mbalimbali uwanjani
 Sehemu ya wadau waliojitokeza kumsikiliza Mbunge Balozi Khamis Kagasheki.
 Wadau wakimsikiliza Mbunge wao kwa umakini.
Hotuba ya Mh. Mbunge imekuza nyanja mbalimbali, kwa kuofia kupotosha tumefanya jitihada za makusudi kukupachikia wewe mdau Msomaji, full audio mwanzo mwisho.
Sehemu ya wadau pichani yupo Dada Pasycazia Barongo na Mzee Faustin Karugendo.
Mshereheshaji Uncle Salum Mawingo(Al Saqry kwa ukoo)  maarufu kama Salum Organizer.
MH.Yusuph Ngaiza pichani kushoto, Ndg Yahaya na Mnec Ndg Karim Amri Amir.
Mchungaji Bililiza akimpongeza Mh. Balozi Kagasheki.
 Nicolas Ngaiza Mtangazaji 88.5 Kasibante Fm Radio akiwajibika.
Mwisho wa Mkutano wananchi wakitawanyika katika viwanja vya Uhuru-Mayunga Uswahili.

HOTUBA NZIMA INAPATIKANA CHINI YA HABARI HII ,PIA VIDEO ZINAPATIKANA JUU YA HABARI HII, INGIA ''OLDER POST 'KWA MATUKIO ZAIDI AU RUDI MWANZA 'KOTE TUPO KAMILI'





Next Post Previous Post
Bukobawadau