Bukobawadau

ZITTO KABWE:HAKI ITAENDELEA TU!!

Mahakama ni Chombo cha kutoa haki. Nimeomba mahakama kuzuia kamati kuu ya chama changu kunijadili mpaka rufaa yangu isikilizwe na Baraza Kuu la chama. Sijaomba kuzuia kamati kuu kuendelea na kikao chake. Nimeomba kamati isinijadili maana nina rufaa kwenda Baraza Kuu kwa jambo hilo hilo ambalo kamati kuu inataka kuliamulia. Wakili wa chama Tundu lissu aliweka mapingamizi akisema mahakama haina mamlaka kujadili masuala ya vyama na wanachama wao. Jaji John Utumwa katupilia mbali mapingamizi yote yaliyowekwa na Tundu Lissu.
Mahakama ndio Chombo cha kutoa haki. Asante Wakili Albert Msando.

Haki itatendeka tu.
Next Post Previous Post
Bukobawadau