Bukobawadau

HAPA NA PALE NA CAMERA YETU MTAANI FEB 6,2014

Camera yetu inakutana uso kwa uso na  Mkurugenzi wa Chichi Hotel Mr Chrithoper Chichi pichani kushoto, kama anavyo onekana akisalimiana na Kaka Mkuu, E.Nyambo mara baada ya kumkabidhi Business Card.
Kama ilivyo kawaida kwa Waungwana wanaonekana wenye furaha huku kila mmoja akimkarisha mwenzake katika Imaya yake,
 Kusshoto ni Mwalimu Roy  Ndema, Zamani alifundisha Mugeza Sekondari, kwa hivi sasa ndiye Mwalimu Mkuu wa  Rwamishenye shule ya Sekondari,kama anavyo onekana akicheck na Camera yetu na Mdau Chrithoper Chichi ambaye ni Mkurugenzi wa Chichi Hotel iliyopo kinondoni B Jijini Dar es Salaam.
 Pichani ni Jengo la TAASISI inayotoa Mikopo kwa Wajasiriamali nchini (Finca)
Muleba Nyumba ya Wageni inayo endelea kuwa na heshima pamoja na kwamba ni ya muda mrefu.
 Anaitwa Nadhir ' Msoja' Kabalabala,huyu ni Mdau mwenye matata mengi watu wa Ilogero kamachumu, Milama  na maeneo ya Uswahili Bilele mtakua mnaelewa ni nini tunamaanisha.
Stand Kuu ya Manispaa ya Mji wa Bukoba.




Taswira stand Kuu ya Manispaa ya Mji wa Bukoba, stand yenye sehemu kuu mbili ya kwanza ni ile yanapopaki mabasi makubwa yaendayo mikoani na nchi jirani,sehemu ya pili ni yanapopaki mabasi madogo au hiace kwa safari za humu Mkoani.
 Tupo na Oxygen Bar& Lounge iliyopo kati ya makutano ya barabara ya jamhuri na Kashozi, mkabala na Bank ya CRDB hawa jamaa wanatikisa na  ndio habari ya mjini.!!



Next Post Previous Post
Bukobawadau