Bukobawadau

ALIYEJIFUNGUA PACHA WANNE AOMBA MSAADA

MKAZI wa Kijiji Chakijage, Kata ya Rwabwere, Wilaya ya Kyerwa mkoani Kagera, aliyejifungua watoto wanne pacha, Jodephina Rugambwa (30), ameiomba serikali kumpatia msaada ili kumsaidia kulea watoto wake.
Akizungumza na waandishi wa habari waliomtembelea nyumbani kwake jana, alisema furaha ya kupata watoto wake hao aliojifungua Machi 23, mwaka huu inaanza kutoweka kwa kuwa anashindwa kuwatunza kutokana na kipato duni alichonacho.
“Mimi na mume wangu ni wakulima wadogo wenye kipato kisichoweza kutusaidia kwa
wakati huu kuwatunza watoto hawa, hivyo tunaomba msaada wa hali na mali kutoka serikalini na kwa wasamaria wema,” alisema.

Alisema mbali na watoto hao wanne, familia yake imejaliwa watoto wengine watatu ambao wawili wanasoma.
Hata hivyo, mama huyo pamoja na mumewe Donati Anatory (38), wameishukuru Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa, wasamaria wema pamoja na wajumbe wa Baraza la Madiwani wilayani humo kwa msaada wao wa hali na mali uliofikia hadi sasa kiasi cha sh 400,000.
Watoto hao pacha, wa kike wakiwa watatu na mvulana mmoja walizaliwa salama wakiwa na afya njema.
Next Post Previous Post
Bukobawadau