Bukobawadau

NI WEMA SEPETU NA HISTORIA YA MAISHA YAKE!!

Akiwa mmoja kati ya wanadada wanofanya vizuri sana kwenye Tasnia hii ya BongoMovies,Wema Sepetu ni msichana  anayetoka kwenye Familia ya kibalozi ni mtoto wa mwisho katika familia ya wasichana wanne wa Balozi Isaack Sepetu Ibrahimu.
 Ana sura na umbo zuri sana, na mvuto mkubwa sana kutokana na rangi yake nzuri ya ngozi… 
Wema sepetu alizaliwa mnamo mwaka 1988 katika hospitali ya ST. Andrew's jijini Dar es Salaam na ni mtoto wa mwisho kuzaliwa katika familia yao yenye watoto wanne wa kike.
Alipata elimu yake ya primary na sekondari katika shule ya ACADEMIC INTERNATIONAL iliyopo jijini Dar es Salaam kabla ya kwenda Nchini Malaysia kusomea mambo ya biashara za kimataifa katka chuo cha Limkokwing University. 
 Pamoja na filamu hizi Wema ameigiza kwenye filamu nyingine nyingi kama Red Valentine, White Maria, Tafrani, Sakata, Crazy Tenant, Diary, Lerato, Dj Benny and Basilisa zilizompatia umaarufu na mafanikio makubwa.
 Pamoja na kuwa na kipaji cha uigizaji wema pia anakipaji kikubwa cha kuimba na pia alishawahi kushiriki mashindano ya urembo na kufanikiwa kutwaa taji la Miss Tanzania mnamo mwaka 2006 na kujipatia zawadi ya gari aina ya Toyota Rav 4. 
Next Post Previous Post
Bukobawadau