Bukobawadau

CAF YAHAHA KUTAFUTA MBADALA WA MOROCCO

Shirikisho la kanda kanda barani Africa CAF linaendelea kuchambua ni nchi gani itakayookoa jahazi ya kuwa mwenyeji wa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2015 baada ya kuthibitisha Morocco kuondolewa rasmi kuandaa fainali hizo.
Nchi ya Morocco imeondolewa kutokana na kukataa kuwa mwenyeji ya mashindano hayo mwakani kwa hofu ya ugonjwa wa Ebola.
Mwandishi wa habari anasema fainali hizo zinaweza sasa kupelekwa Angola nchi iliyokuwa mwenyeji wa fainali hizo miaka minne iliyopita.
Nchi nyingine zinazodhaniwa kuweza kuandaa mashandano hayo ni Gabon na Nigeria. Shirikisho la kanda kanda barani Afrika linasema litatoa uamuzi ni nchi ipi itakayoandaa mashindano hayo haraka iwezekanavyo.
Next Post Previous Post
Bukobawadau