Bukobawadau

MATUKIO KATIKA PICHA WILAYANI NGARA

LEO wafanyakazi na watumishi wa radio Kwizera kituo cha ngara mkoani Kagera na Kigoma wamekutana na uongozi wa  wa Radio hiyo luweka mipango ya Pamoja kufanikisha utafutaji na utoaji habari kwa jamii inakosikika radio hiyo hadi nchi jirani za maziwa makuu,
Pichani ni watumishi wa Radio Kwizera Mkoani Kagera Kigoma na DRC wakiwa  na Mkurugenzi wa Radio Kwizera Fr Damas Misanga.
 Mkurugenzi wa Radio Kwizera Fr Damas Misanga pichani amewataka wanahabari katika vituo wanakofanyia kazi  kuthamini kwanza usalama wa maisha yao na kufuatilia habari baadaye kwani wanaweza kuwa chambo cha na kupoteza maisha yao
Katika matukio makubwa yaliyoko mbele mwaka huu ya uandikishaji wapiga kura katika daftari la wapiga kura , maoni ya kupitisha katiba iliyopendekezwa, kampeni za uchaguzi mkuu hadi kuwapata madiwani wabunge na Rais
Fr Damas Misanga kawataka wanahabari hao kuhakikisha wanatoa habari ambazo sio za uchochezi  na kuwapa nafasi wanaolalamikiwa kutoa maoni yao bila kutumiwa na wanasiasa kwa maslahi yao binafsi
Amesema kuwa habari nyingine lazima kabla ya kufikishwa radioni kuwe na uchunguzi na kuhoji mamlaka husika ili kila mmoja kupata haki yake kwa kukuza demokrasia na utawala bora
Mwezi Machi Kituo cha Radio Kwizera kina tarajia kuenea kwa kupanua matangazo yake katika mikoa ya Kagera Mwanza Geita hadi wilaya ya Kahama ikiwemo mikoa ya Rukwa na Katavi.
 Watumishi wa Radio Kwizera Mkoani Kagera Kigoma na DRC wakiwa  na Mkurugenzi wa Radio Kwizera Fr Damas Misanga katika picha ya Pamoja
 Habari na picha By Shaaban Ndyamukama
Next Post Previous Post
Bukobawadau