Bukobawadau

WAZAWA WA MKOA WA KAGERA WAISHIO NJE YA MKOA WAJIPANGA KUUREJESHA MKOA HUO KATIKA ENZI ZA NSHOMILE

 Baada ya kilio cha muda mrefu kwa wazawa wa Mkoa wa Kagera  ambao wanaishi nje ya mkoa huo na wasomi na wenye uwezo mkubwa kiuchumi kukumbushwa kila mara kurudi nyumbani kuwekeza na kuinua uchumi wa mkoa wao,  wanakagera hao sasa wameanza kuitikia wito huo kurudi nyumbani.

Wanakagera hao ambao wanaishi nje ya Kagera  wameunda  umoja wao ambao unajulikana kama Friends of Bukoba na kuanza kuweka mikakati ya kuukumbuka mkoa wa Kagera ambako ni kwa kwao ili uendane na sifa yake kama ilivyokuwa miaka ya 1970.

Kutoka kila kona ya dunia Wanakagera sasa wameamka ili kuurejeshea mkoa wa Kagera jina lake la NSHOMILE lakini kufuta nshomile but no course, hayo yamebainika baada ya wazawa wa Mkoa wa Kagera kupitia Friends of Bukoba kuanzisha mfuko  wa maendeleo wa mkoa.

Wazawa wa Mkoa wa Kagera wakiongozwa na Mzee Kamzola kupitia Friends of Bukoba wanasema kuwa tayari wamechangia shilingi milioni 500 na kipaumbele chao ni Elimu kwanza ili kufuta ujinga katika kizazi cha sasa cha mkoa wa Kagera na kuwa nshomile kama zamani.

Hayo yalibainika mara baada ya Siku Kuu za Mwisho wa mwaka 2014 zilizowakusanya Wanakagera wengi waliokuja kusherekehea na familia zao Mkoani humo. Mapema Januari 2015 wanakagera hao walianza mikakati ya kukutana  na wanakagera wanaoishi ndani ya Kagera kuweka mpangokazi wa pamoja.
Wakikutana na Mkuu wa Mkoa katika ofisi yake pamoja na wadau wa maendeleo wa mkoa waliweka mikakati na kubainisha kuwa mkoa wa Kagera hapo miaka ya 1970 ulipata umaarufu kwasababu ya elimu na kwa sasa elimu imeshuka kwa kiwango kikubwa.

Wanakagera kupitia Friend of Bukoba walibaisha kuwa tayari wao wameamua kuanza na elimu lakini wanawashirikisha wadau wengine waishio mkoani hapa jinsi ya kukukuza kiwango cha elimu na uwekezaji katika Nyanja nyingine utafuata baadae.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera John Mongella alisema suala hilo lazima liwashirikishe wadau wengi ili kusije tokea matatizo mbele ya safari. Pia wananchi waishio ndani ya mkoa kuwa tayari kuchangia katika kuuendeleza mkoa wao na si kuwategemea waishio nje ya mkoa pekee katika maendeleo.

Wito, wewe mzawa wa mkoa wa Kagera unakumbushwa kupakumbuka nyumbani kwa maendeleo ya mkoa wako uweze kukua kiuchumi.
Next Post Previous Post
Bukobawadau