Bukobawadau

MTAZAMO WA MDAU KUHUSU KARAGWE YETU !

 My home!!Thanks for the blog post. I am very nostalgic right now. Karagwe has so much potential to build the Tanzanian economy from the game reserve (burigi) that is a tourist attraction, coffee plantations that have been the source of income for many of our parents, Pastoralism which if we took advantage of would be generating income and empolying many young people for example if a dairy Farm was to be started in that region.
 I am disappointed when Tanzanians are so busy importing milk from South Africa and many youth stay unempolyed when cows are being killed in big numbers kwenye "operations"za kijinga! What happened to Kikurura Ranch? Karagwe has a rich history Yes but is it as developed as it ought to be? Sadly over the years Karagwe inarudishwa nyuma. I visited my home after a long time away and i was dissapointed by their leaders "Wabunge"! So many houses destroyed for "road construction" which has been the song ever since i was born, the project is on going but i am afraid my.
Naye Mdau Frank Johnson pichani ametoa majibu ya maoni ya mdau kupitia ukurasa wetu wa Facebook anasema;Huyo mdau anaolalamika baada ya kupotea kwa muda mrefu bila kwenda kwao na kukuta mambo sivyo alivyotarajia naomba nimjibu kama ifuatavyo:
Huwezi kuwa unalalamika tu bila kufanya jitihada zozote zako binafsi kuendeleza sehemu uliyotoka,maendeleo yataletwa na watu wenyewe wa uko hasitegemee wageni waje kumletea mabadiliko.
Kuhusu game reserve ( burigi) huyo mdau amechukua jitihada gani binafsi kutangaza utalii wa kwao ili wananchi wa uko wapate kipato.Yeye pia ana jukumu la kutangaza huo utalii.
Kulalamika tu wakati ukijua haukuwa sehemu usika na haujachukua jitihada zozote binafsi hakutoshi pia haisaidii.
 Pia huyo mdau muulize jitihada gani amechukua kuelimisha jamii yake ya wakulima na wafugaji namna ya kutumia rasilimali waliyonayo kujikomboa,maana tumeshuhudia watu wana ng'ombe zaidi ya 5,000 lakin bado ni masikini.Je anampango gani kwenda kuwaelimisha badala ya kulalamika tu bila yeye kufanya kitu.
 Maoni yangu ni kuwa kama mtu umeondoka kwenu muda mrefu bila kurudi na haujachukua hatua zozote kuendeleza siku ukirudi kwenu ukakuta mambo yamearibika zaidi usimlalamikie mtu sababu mwenye jukumu la kuleta mabadiliko ni wewe mwenyewe,na mifano mingi sema nisiwachoshe kuonyesha watu ambao wako vizuri sana sehemu nyingine lakin wameshinda kuendeleza wanapotoka na badala yake wanaishia kulalamika tu ninachosema hakuna mtu mwingine zaidi wa kuleta mabadiliko ni wewe au sisi .
Ni hayo tu
by Mdau
Frank Johnson


Next Post Previous Post
Bukobawadau