Bukobawadau

MAASKOFU WAWATAKA WAKRISTO KUWA WATULIVU WAKATI SAKATA LA ASKOFU GWAJIMA LIKISHUGHULIKIWA KISHERIA.

Siku moja baada ya kiongozi wa kanisa la ufufuo na uzima kuachiwa kwa dhamana na jeshi la polisi, maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali wameibuka na kuwataka wakristo kote nchini kuwa katika hali ya utulivu wakati sakata la askofu Josephat Gwajima likishughulikiwa na vyombo vya sheria.
Wakizungumza jijini Dar es Salaam na vyombo vya habari, maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali, licha ya kukataa kusema walichozungumza na mkuu wa jeshi la polisi nchini, wamewataka wakristo kote nchini kuwa katika hali ya utulivu huku wakiendelea kuenzi tunu ya amani iliyopo hapa nchini wakati vyombo vya sheria vikiendelea kushughulikia sakata hili la askofu Josephat Gwajima.
 
Wakizungumzia kauli ya askofu Gwajima aliyotamka kwa vyombo vya habari wakati akitoka kuhojiwa katika kituo cha polisi cha Osterbay jijini Dar es Salaam kuhusu kusimamia kauli zake, maaskofu hao wamesema kwamba askofu Gwajima hawawezi kusaliti kauli iliyotolewa na jukwaa la waakristo Tanzania na akifanya hivyo hata wao watamshangaa na ndio maana askofu Gwajima aliwaambia waandishi wa habari kwamba yeye kama mtumishi wa mungu lazima akemee jambo analoona haliendi sawa.
 
Maaskofu hao na wachungaji wamempongeza kwa dhati askofu mkuu wa jimbo kuu la Dar es Salaam Cadinali Polcarp Pengo kwa kutangaza kusamehe yote yaliyotokea kati yake na askofu Josephat Gwajima kwani kwa kufanya hivyo ndio ukiristo wa kweli.
Next Post Previous Post
Bukobawadau