Bukobawadau

CHUMBA CHA HABARI CHA GAZETI LA JAMBO LEO NA STAA SPOTI CHAZIZIMA KWA HUZUNI BAADA YA KUFIWA NA MENEJA WAO MZEE RAMADHANI KIBANIKE

 Marehemu  Ramadhani Kibanike enzi za uhai wake.
 Mhariri Mkuu wa Gazeti la Jambo Leo, Julian Msacky na Mwandishi wa Habari, Stela Kessy (kulia), wakiendelea na kazi huku wakiwa na hudhuni baada ya kupokea taarifa ya kifo cha Kibanike leo jioni.
 Mwanahabari Celina Mathew akilia kwa uchungu baada ya kupokea taarifa hiyo.
 Ofisa Matangazo, Kinai akiwa amepigwa butwaa kutokana na  kifo hicho.
 Wanahabari Nyendo Mohamed (katikati), Edith Msuya (kulia) na  Magendela Hamisi wakiwa katika hali ya huzuni kufuatia kifo hicho.
 Mwanahabari Magendela Hamisi akitafakari juu ya kifo hicho.
 Msanifu kurasa wa gazeti la Jambo Leo, Elizabeth Mkeleja alishindwa kujizuia kulia.
 Dereva wa Ramadhani Kibanike akiwa katika huzuni baada ya kupokea taarifa ya kifo hicho.
Mwanahabari Grace Gurisha akisaidiwa na wenzake baada ya kuishiwa nguvu muda mfupi baada ya kupata taarifa hizo za kifo cha Meneja  Ramadhani Kibanike.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya JL Comunications inayochapisha magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti, imepata pigo baada ya aliyekuwa Meneja wake Mkuu Ramadhani Kibanike kufariki.

Kibanike amefariki dunia leo mchana nyumbani kwake Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Akitoa taarifa ya kifo hicho kwa wafanyakazi wa Kampuni hiyo, Mkurugenzi wa Kampuni hiyo Theophil Makunga alisema Kibanike alikumbwa na mauti leo mchana.

Taarifa hiyo ambayo iliwashtua wafanyakazi wa Kampuni hiyo na hata kupelekea baadhi yao kupoteza fahamu, ilisababisha pia kusimama kwa muda kwa shughuli za Kampuni hiyo.


Mipango ya mazishi bado inapangwa, na msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata Jijini Dar es Salaam. (Imeandaliwa na mtandao wa www. habari za jamii.com- simu namba 0712-727062)
Next Post Previous Post
Bukobawadau