Bukobawadau

MAADHIMISHO YA SIKU YA UTALII DUNIANI BUKOBA JUMAMOSI SEP 26 ,2015

KIONGOZI WA MAANDAALIZI: KIROYERA TOURS. ( WADAU WOTE PIA WANAKARIBISHWA ).KAULI MBIU YA MWAKA HUU : “MAMILIONI YA WATALII NI MAMILIONI YA FURSA.”
 LENGO NI NINI?
Umuhimu wa kuadhimisha siku ya utalii duniani ni kuhamasisha uelewa katika jamii juu ya mchango wa utalii katika maendeleo ngazi ya familia na mtu binafsi, kitaifa na kimataifa. Hii ikiwa katika nyanja nyingi ikiwemo  kiutamaduni, kisiasa, kijamii na kiuchumi.
Siku ya utalii duniani huadhimishwa kila mwaka tarehe 27 Septemba. Serikali ya Tanzania ni mwanachama wa Umoja wa mataifa na hivyo huadhimisha siku mbali mbali ambazo zinatambuliwa na Umoja wa Mataifa kama siku ya Mazingira Duniani, Siku ya wafanyakazi duniani na hivyo  husherekea siku hii pia. Wadau wa sekta husika husaidiana na Serikali kuadhimisha siku kama hizi na pia tarehe ya siku ya maadhimisho yaweza kubadilishwa kidogo kama kuna umuhimu wa kufanya hivyo.
HISTORIA YA SIKU HII MJINI BUKOBA:Mji wa Bukoba ulianza kuadhimisha siku ya utalii duniani  mwaka 2002 na kuendelea kufanya hivyo  kila mwaka hadi mwaka 2008.
Kulikuwa na chama cha kuendeleza utalii mkoa wa Kagera maarufu kama Kagera Tourism Development Association ( KATODEA) ambacho kilifanya mchango mkubwa na  katika mwaka 2006,  Mkoa wa Kagera ulipata fursa adimu ukawa mkoa ulioadhimisha siku ya Utalii Duniani kitaifa hapa mjini Bukoba. Huo ndio ulikuwa ufunguo wa kutambuliwa Mkoa wa Kagera katika ramani za utalii nchini Tanzania. KATODEA imekuwa haiendelei  kwa muda mrefu sasa.
UMUHIMU WA KUSHERERKEA SIKU YA UTALII DUNIANI BUKOBA
Kuanzia mwaka 2002 utalii ulikua na kuanza kuleta mabadiliko endelevu mwaka hadi mwaka. Mahoteli  kama Walkgard, Kolping, Victorious Pearch, Smart, Yaasila Top kwa sasa Bukoba Coop na nyingine nyingi zilijengwa. Kiroyera Tours, Walkgard hotel, Tausi Curio na Hoteli ya Kamachumu Inn walikuwa mstari wa mbele kutangaza utalii. ‘Tausi curio shop’ ilikua haraka na kuwa na maduka matatu yenye kazi za mikono ya hali ya juu na ya kuvutia watalii  katika mji wa Bukoba.  Watalii walianza kutembelea vivutio mbali mbali vilivyoko Manispaa ya Bukoba, Bukoba vijijini, wilaya ya Muleba na wilaya ya Misenyi.
Kazi kubwa ilifanywa ya kuainisha vivutio mbali mbali vilivyomo Mkoani Kagera kwa msaada wa wizara ya mali asili na utalii. Vivutio pia viliendelezwa kwa kuwekewa barabara za kupitia watalii, kutengeneza ratiba za matembezi zinazounganisha vivutio hivyo na kuvitangaza katika maonesho mbali mbali kama saba saba hapa Bukoba na maonesho ya utalii kitaifa (huko Arusha na Dar es Salaam) pia maonesho ya kimataifa (Spain, Uingereza, Milani, Belgium, Ufaransa na Marekani). Vijitabu vya vuvutio hivi viliandikwa  pia na kusambazwa.  Katika vivutio hivi kuna mvuto wa Ziwa Victoria kwenda kisiwa cha Musira,  kisiwa cha hifadhi ya Rubondo (Rubondo Island National Park) na vinginevyo. Kuna msitu wa Kyamunene na  maporomoko ya maji na pango karibu na Bukoba na maporomoko yam to Bugonzi huko Kamachumu; Wahunzi wa vyuma wa Itahwa na utaalamu wa asili wa vyuma wa Maruku Zamadamu Katuruka; Mapango ya michoro ya kale ya Bwanjai –Mugana; chakula na mapishi ya asili, ngoma na nyimbo za kitamaduni Gera, maarufu kama” kwa mama Kisha”  na nyumba za asili za “majani full suit” maarufu kama “Mushonge museum” huko Kanoni   Kamachumu. Kwa juhudi hizi Kisiwa cha Rubondo ambacho hapo awali kilikuwa kinapata wageni kwa nadra sana, kwa sasa huwa kinafikia kukataa kupokea wageni ili kulinda kisizidi viwango na kuathiri uhifadhi wa wanyama na mazingira.
UKUAJI WA UTALII MJINI BUKOBA
 Ni vyema kusema Bukoba inapokea watalii halisi kutoka nje 2000 kwa mwaka, ambao wanafika  Bukoba kwa ajili ya utalii tu. Kati ya hawa kuna wanaotaka kuona na kutembelea vivutio vilivyopo hapa Bukoba, na baadhi yao ni wapita njia, wengine wanatafuta usafiri, wengine wanatafuta huduma ya malazi na baadhi wanataka kuishi kwa muda katika jamii ya Bukoba na kufanya kazi za kujitolea. Ni mara nyingi sana kuona magari yakusafirisha  watalii kutoka Uganda na Rwanda yakiwa Bukoba. Ukweli ni kuwa nchi ya Uganda hupata watalii wengi kuliko nchi ya Tanzania. Baadhi ya watalii kutoka Uganda hupitia mjini Bukoba wakiwa wanaelekea kwenue mbuga za wanyama za Serengeti na Ngorongoro. Huduma ya usafiri ni muhimili kwa utalii. Wasafirishaji ni pamoja na kampuni ya ndege ya Auric, Precision Air,  huduma za usafiri wa majini MV Victoria na sasa MV Serengeti  ambayo kwa sasa ni chaguo la watalii wengi wa Bukoba. Pia kuna usafiri wa njia ya barabara Taxi pamoja na mabasi na boda boda.
 AJIRA KATIKA UTALII
Kwa makadirio ya kuwa watalii 15 hutengeneza ajira ya mtu mmoja, Tuseme angalau wakazi 100 wa Bukoba wana ajira ya moja kwa moja kwenye utalii kama mahotelini na katika kampuni za utalii. Tukikadiria kwa wastani  muajiriwa mmoja anawategemezi watano, ni dhahiri kuwa takribani watu 500 hapa Bukoba wanategemea utalii katika maisha yao.
Biashara ya Utalii inategemea sana Nyanja nyingi za ugavi (Supply chain) kwa mfano wauza vyakula wa soko kuu, maduka yanayouza bidhaa mbali mabali kama taa, dawa za miswaki, sukari na vifaa vya ujenzi. Watoa huduma ya burudani pia wanahitajika kama ajira. Wakulima wa mbogamboga, matunda, na maua na wafugaji wa kuku na ng’ombe. Pia wauzaji wa mavazi, mashuka na vitambaa vya meza za chakula, glasi, sahani, uma, visu pamoja na vijiko n.k.  huduma za vinywaji baridi na vikali, wauza vinyago, wachapishaji wa vipeperushi na internet cafĂ©, makampuni ya ulinzi, na wanausalama wote, hawa wote ni wadau wa utalii na wanapatikana hapa Bukoba.
Tukiunganisha waajiriwa katika Utalii na wale wanaonufaiuka na utalii kupitia ugavi, tunasema wako watu takribani 1000 wanaopata ajira  kutokana na sekta ya utalii.
JE NI KWA JINSI GANI MAADHIMISHO YATAFANYIKA  MJINI BUKOBA?
TAREHE: Siku ya maadhimisho itakuwa Jumamosi 26 Septemba 2015
MAHALI: Ni katika viwanja vya Kiroyera Tours vilivyoko katika fukwe za ziwa Victoria, barabara ya        Forodhani – Shore Road Kata Bakoba
SHUGHULI:
   1. KONGAMANO (ROUND TABLE): Kutakuwepo na kongamano litakalochukua masaa 2 (mawili) na litaendana na Kauli mbiu ya mwaka huu inayosema “Mamilioni ya watalii ni Mamilioni ya fursa”.Maongezi yataendana na maana nzima ya utalii endelevu; Utalii unaolenga  kuondoa umasikini, Ukuzaji wa ujasiliamali na uwekezaji; teknolojia na ufundi na Huduma bora kwa watalii ( Excellence in Customer care). Wazungumzaji watatokana na wadau. Maswali na majibu yatakuwepo.
2. MAONESHO:   Kutakuwepo na maonesho mbalimbali ya bidhaa zinazotengenezwa na kuzalishwa na wadau wa utalii kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Kagera. Bidhaa hizo ni pamoja na za hoteli za kitalii, vivutio vya watalii, wafanyabiashara wa utalii Tanzania, wasafirishaji na watoa huduma ugavi kama TANICA, wauza  vinywaji na kazi za mikono wanakaribishwa. Wadau wa utalii wote wote watakaribishwa kufanya maonesho yao siku hiyo na kwa wanaohitaji meza ya maonesho italipiwa elfu 20 tu.
3. MAANDAMANO YA MAGARI NA PIKIPIKI: Tutawakaribisha wapanda pikipiki 30 na magari kuzunguka mitaa ya manispaa ya Bukoba kuonesha umuhimu wa sherehe ya utalii  Duniani na watu wote watakaribishwa kushiriki sherehe hiyo.
4. KUTOA  ZAWADI: Aina tatu za huduma ya utalii zitatambuliwa na kutunukiwa vyeti maalum.
 sekta zitakazotambuliwa ni: Hoteli tatu, kampuni za usafirishaji tatu na vivutio vya watalii vitatu.
5. KUZINDUA JIWE LA KUMBUKUMBU YA MJERUMANI EMIN PASHA NA KUANZA KWA MJI WA BUKOBA MWAKA 1890
6.NYAMA CHOMA: Nyama choma pamoja na muziki na kucheza ngoma vitakuwapo.
Media: Watakaribishwa waandishi habari na wapiga picha za video na bloggers.
SERIKALI: Kutakuwepo na viongozi wa serikali akiwamo mgeni rasmi na TANAPA, Uwakilishi wa wizara husika,  Tanzania Tourist Board (TTB) nk. Viongozi hawa watashiriki katika maadhimosho haya  kwa ufunguzi rasmi, ushiriki katika kongamano, Ushiriki katika maonesho, maandamano na shamra shamra ikiwemo hotuba rasmi kwa wananchi wote.
NATANGULIZA SHUKRANI.
Imetayarishwa na MARY CONSO KALIKAWE , Mkurugenzi Mwendeshai KIROYERA TOURS.
Kwa mawasiliano: +255 713526649 au barua pepe:  mkalikawe@gmail.com   
KIROYERA TOURS ALWAYS PUTS YOU FIRST! 
MPANGO WA MAONESHO SIKU YA UTALII DUNIANI 26 SEPTEMBER 2015
VIWANJA VYA KIROYERA TOURS BUKOBA
     Kutakuwa na Mahema matano 5 yatakayokuwa yametazama ziwani kwenye sehemu ya uwazi iliyoko kati ya Ofisi za Kiroyera Tours na upande wa Bar.

2.       Ndani ya kila hema kutakuwa na meza nne ambazo kutakuwa na kampuni, watu binafsi au taasisi

3.       Jumla ya watakaokuwa wanaonesha ni takribani unit 25 ambazo ni  zifuatazo

i)        Rubondo Island National Park TANAPA
ii)       Tanzania Tourist Board (Mwanza Regional Office)
iii)     Department of Tourism (MNRT DSM)
iv)     SAA NANE Island National Park
v)      Regional Office (RAS Kagera)
vi)     BMC (Bukoba)
vii)   Kyamunene water falls and Cave (Rubale Forest Bukoba)
viii)  Kolping Hotel
ix)     KAPOTIVE singers
x)      Kagera Museum
xi)     Mama Kisha cultural Gera
xii)   Mushonge Museum Kamachumu
xiii)  Thereza Ntezibwa Women Crafts
xiv) Humpton’s CafĂ© (Bukoba)
xv)   WalkGard Hotel
xvi) Karume Day Primary School
xvii)            CRDB Bank
xviii)          Kiroyera Tours
xix)             Victorious Perch Hotel
xx)               Zamadamu - Katuruka Iron Technology and cave of the dead
xxi)             Itahwa Wahunzi wa Vyuma
xxii)            ELCT Hotel
xxiii)          Auric Air
xxiv)          TANICA
Kila mshiriki  anategemewa kulipia ushiriki wa naonesho angalau elfu 20. Wale wakubwa tumewawekea elfu 50 au laki moja kama gharama ya kushiriki. Hii itachangia kidogo katika gharama za sherehe hii.
 JE KIROYERA TOURS NI NANI?

Mary Passpot Photo 2.jpgKiroyera Tours ni kampuni iliyosajiliwa BRELLA mwaka 2001 kwa Reg No… . Ina leseni ya kuongoza watalii TALA….  Kampuni hii ndio ya  kwanza kuanzisha utalii mkoani Kagera ikiwa imeanzishwa na wanawake watano wazawa wa mkoani humu. Makao makuu yake ni hapa mjini Bukoba hata ingawa imefungua tawi huko Dar es Salaam. Kiongozi wa wanawake hao ambaye ni mkurugenzi mtendaji wa Kampuni hiyo anaitwa Bibi Mary Kalikawe. Bibi Mary Kalikawe ni mtaalamu wa mambo ya utalii na alikwisha ajiriwa na Serikali ya Botswana kwa miaka mingi kama Expatriate mtanzania kabla hajarudi Bukoba kufungua kazi za kampuni hii. Pia mama huyu ameshafundisha chuo kikuu cha Dar es Salaam.  Maneja wa sasa wa Kiroyera Tours ni Aaron Kalikawe. Kampuni ina wafanyakazi 15. Kati yao ni Bw. Superius Kalemera ambaye ni muongoza watalii mzoefu wa miaka mingi, Bi Methodia Method Maneja wa Kagera Museum na wengineo. Tafadhali tembelea tovuti ya Kampuni www.kiroyeratours.com na brochure yetu kwa ufahamu zaidi.

1.0 VIVUTIO VYA UTALII
Mama Mary akiwa anaongoza kampuni hii ameweza kuteuliwa kuwa mkurugenzi wa Tanzania Tourist Board TTB na kampuni imeweza kupata tuzo mbali mbali za kimataifa na kitaifa ikiwemo ya Spain Millenium Tourism Award, UN Habitat Nairobi,  Ford Foundation, World Bank iliyotolewa nchini Ghana na nyingine nyingi. Juhudi za Kiroyera Tours zilifanya mkoa wa Kagera uwe na chama bora cha Utalii kikiitwa Kagera Tourism Association. Kiroyera Tours licha ya kuanzisha kampuni ya kwanza ya utalii ambayo imedumu kwa miaka 14 sasa hapa mjini Bukoba, ilifungua Kagera Museum iliyoko Nyamkazi na camping site iliyoko ufukweni shore Road. Imevumbua na kuendeleza vivutio mbali mbali vya Utalii hapa Mjini Bukoba ikiwemo kisiwa cha Musila, Maporomoko ya msitu wa Rubale Kyamunene, Maandishi ya kale ya Bwanjai, Kamachumu, Gera, ulimaji wa kahawa na vanilla kwa watalii nk. Kwa kazi hizi Bibi Mary Kalikawe aliwahi kuteuliwa akawa Mkurugenzi wa bodi ya Utalii TTB. Juhudi za Kiroyera zimetangazwa kwenye vitabu vya kimataifa vya kuongoza watalii kama Lonely Planet, Brandts Guide,  magazeti mbali mbali na vyombo kadhaa vya habari. Kiroyera imepokea na kutembeza watalii kutoka nje ya nchi takribani elfu Tatu tangu kuanza kwake. Kampuni inazidi kuvumbua na kuunda vivutio zaidi.
2.0 DIRA YA KAMPUNI (Imeandikwa kwa kiingereza)
2.1  Mission
The Mission of Kiroyera Tours and Consulting is to widely promote Lake Victoria Zone in particular Kagera Region as a tourist destination and to operate quality assured tourism services within the Lake regions and around Dar es Salaam and beyond. Through our consultancy services, to contribute to capacity building and ensuring Kagera and other areas of Tanzania make the most of their Natural assets now and for the future. 
2.2 Vision
To sustain Kiroyera Tours and consulting as a leader in Tourism Development in the East Africa region by maintaining a high rank among the best companies and a preferred choice for tourists and other clients.
 Tafadhali angalia kijitabu cha “COMPANY PROFILE” Kiroyera Tours kwa maelezo zaidi.
3.0 USHIRIKISHAJI WA WANANCHI KATIKA UTALII
Kampuni ya kiroyera imefanya bidii sana kuhusisha wananchi katika faida zinazoletwa na utalii. Tangu kuanza kwake Kiroyera
3.1 Ajira:  imeajiri wafanya kazi wazawa peke yake hata ingawa imebahatiwa kuwa na Volunteers wengi kutoka nchi mbali mbali. Hawa wameleta na kubadilishana ujuzi na wafanyakazi waliowakuta. Wafanyakazi wote wamejifunza kuendesha huduma za utalii wakiwa wameajiriwa ndani ya kampuni. Tangu kuaza kwake Kiroyera tours imekwisha ajiri wafanyakazi zaidi ya 50 wengine wamehama na kutafuta kazi mahali pengine. (Kuna waliajiriwa na kampuni kuubwa kabisa za utalii kutoka Ulaya na Marekani kama Grumeti (Justin Mwabuki), Asilia (Hamza), wengine wamepata kazi serikalini (Mariana na Zaharani) na wengine wameanzisha kampuni zao wenyewe za utalii akiwemo Bi Mariana wa Mama’s Travel Agency ya Mwanza yenye tawi Bukoba na Bw William Rutta aliyekuwa Maneja wa Kiroyera ambaye ameanzisha kampuni ya Bukoba Cultural travel.
3.2 Kukodi vifaa vya kazi kutoka kwa wanachi: Baiskeli za kuzungusha watalii mjini Bukoba na mitumbwi ya kuzungusha watalii ziwani  huwa zinakodiwa wananchi wenyewe. Mara kwa mara tunakodi magari ya kutembeza watalii kutoka kwa wakazi wa mjini Bukoba. Usafiri wa ndege, meli, mabasi, daladala, pikipiki pia. Hoteli mbali mbali, migahawa na guest house ni wadau wetu tunapolaza watalii na kupata chakula cha watalii. Vivutio vya utalii tunatumia vilivyopo katika sehemu za wananchi na tunakwenda hadi mabali Kamachumu, Mugana, Gera, Missenye nk. kupeleka watalii na kulipa watu wenye vivutio vyao huko.
3.3 Sokoni, madukani, vifaa vya ujenzi, mafundi, simu na mawasiliano pia wataalamu (Accountants): Fedha ambazo zimepitia Kiroyera zikaingia sehemu hizi mbali mbali zinazidi wastani wa milioni 12 kwa mwaka
3.4 Kodi kwa Serikali na michango katika jamii: Kiroyera Tours ni kampuni pekee inayolipa USD 2000 kila mwaka kwa leseni halali ya kuongoza watalii na kutimiza masharti yote yanayotakiwa na serikali kupewa leseni hii. Tunalipa TRA vema kabisa na hata NSSF na ushuru mbalimbali wa Manispaa. Jamii imeichagua Kiroyera Tours kuwa mahali pa kuzungukia wakiwa wanachagisha michango ya kila aina!
4.0 WATOTO YATIMA NA WALEMAVU         
Kampuni ya Kiroyera imejihusisha na kuanzisha NGO’s za kusaidia walemavu kama BUDAP (www.budap.org) na Heritage Initiative Bukoba ambayo imechangia sana kutunza watoto yatima. NGO’s hizi zinajulikana kitaifa na kimataifa.  Uwezo kusaidia jamii kutumia NGO’s hizi umetokana na watalii wanaopitia kampuni yetu.



Next Post Previous Post
Bukobawadau