Bukobawadau

Jameson yaandaa pre-party George and Dragon Dar kuelekea Jameson Live Party itakayofanyika Nairobi.


  • Mshindi mmoja kujishindia tiketi ya watu wawili kwenda Kenya kwenye party ya Jameson itakayotumbuizwa na B.O.B

Jameson inaandaa pre-party itakayofanyika tarehe 21 ya mwezi huu katika bar ya George and Dragon jijini Dar es Salaam.
Watumiaji wa Jameson watakaonunua chupa ya kinywaji hicho watafanikiwa kuingia moja kwa moja kwenye droo ya kushinda tiketi ya kwenda Kenya kushuhudia party ya Jameson itakayofanyika hapo tarehe 12, December.
Jameson Live 2015 Party, inamleta msanii wa hiphop kutoka Marekani, Bobby Ray Simons, maarufu kama B.O.B, ambayo itafanyika Ngong Racecourse hapo tarehe 12 December.
Rapa huyo mzaliwa wa Atlanta amezungumzia kuhusu show yake hiyo ya Nairobi katika ukurasa wake wa Facebook, akiwataka mashabiki wake wajiandae kwa show kali.
B.O.B ambaye alitambulika katika ulimwengu wa muziki kupitia kupitia mixtape yake ya Cloud 9, amefanikiwa kufanya show sehemu mbalimbali duniani huku wimbo wake wa ‘Airplanes’ na ‘Nothing on You’ aliyomshirikisha Bruno Mars zikiongoza chati mbalimbali za mziki duniani.
Nyimbo zake za hivi karibuni kama ‘So Good’ na ‘Headband’ nazo zimefanikiwa kumfanya B.O.B kuwa mmoja ya wanamuziki wakubwa duniani.

Huku akiwa ameshinda tuzo mbalimbali za BET, MTV pamoja na Teen Choice na huku akifanikiwa kuchaguliwa kuwania tuzo za Grammy zaidi ya mara sita, B.O.B ameshawahi kufanya show na wanamuziki mahiri kama Janelle Monae, Eminem, Linkin Park, Kanye West, Drake, Usher, Paramore na wengine wengi.

Jameson wamejipanga kukuza viwango vya burudani kwa nchi za Afrika Mashariki na awamu hii wamejipanga kwa kuwapa burudani ya pekee mashabiki watakaohudhuria burudani hiyo huku wakizidi kuwekeza zaidi katika kuwaleta wasanii wa kimataifa.
                                                                                            
Mwaka 2014 Jameson ilifanikiwa kuandaa matamasha mawili makubwa nchini Kenya ambayo yote tiketi zake zilimalizika kabla huku la kwanza burudani ikitolewa na wasanii wa ndani, na la pili burudani ilitolewa na msanii 2 Chainz huku balozi mashuhuri wa Afrika Akon akihudhuria pia.

Akizungumzia kuhusu show hiyo, Balozi wa Jameson, Antony Owich amesema party ya mwaka huu itazidi kuwa kubwa na bora kuliko miaka iliyopita.

‘Jameson imejikita katika kuwapa kumbukumbu za kipekee mashabiki wake na kwa mwaka huu inawaahidi kuwapa burudani ya pekee kabisa na watu wasikose kuhudhuria’ alisema Owich.







Next Post Previous Post
Bukobawadau