Bukobawadau

MAKONTENA ZAIDI YA 2400 YAPOTEA!!

Mengine fasta๐Ÿ˜„๐Ÿ˜„
UPDATE
Waziri mkuu, Kassim Majaliwa ametembelea bandarini na shirika la reli Tanzania(TRL). Akiwa bandarini amekagua mfumo wa utoaji na uingizaji mizigo bandarini. Katika maongezi ya awali meneja wa bandari alimuhakikishia kuwa mfumo hauruhusu kontena kuibiwa lakini waziri mkuu alienda na ripoti ya ukaguzi na kumuonyesha majina ya waliopitisha makontena zaidi 2400 bila kulipiwa kodi, amempa muda wa masaa matatu hadi saa kumi na mbili jioni aambiwe hatua zilizochukuliwa kwa wahusika kwa sababu anawafahamu.

Katika hatua nyingine, waziri mkuu alitembelea shirika la reli na kukuta mabilioni yametumika na miradi iliyokusudiwa haijatekelezwa.
Next Post Previous Post
Bukobawadau