Bukobawadau

MPANGO WA OFISI YA WAZIRI MKUU KUHAMIA DODOMA WIKI IJAYO WAKAMILIKA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Uratibu, na Watu Wenye Ulemavu) Jenista Mhagama (Mb)amepokea  Mpango Mkakati  wa Kuhamia Dodoma  wiki ijayo wa Ofisi ya Waziri Mkuu leo Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Julai,2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo.
Mhagama amekutana wna wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi katika kukamilisha Mpango Mkakati huo ili kukamilisha utekelezaji huo. 
 Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali akiwasilisha Issa Nchasi akiwaitisha wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi za Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye Mpango wa Ofisi hiyo kuhamia Dodoma wiki ijayo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Jenista Mhagama na Naibu Waziri anayeshughulikia ( Watu Wenye Ulemavu )Abdallah Possi  pamoja na wakuu wa Idara wakifuatilia uwasilishwaji wa Mpango Mkakati wa Kuhamia Dodoma wa Ofisi hiyo, leo  Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Julai, 2016.
 Wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa Mpango Mkakati wa Kuhamia Dodoma leo Jijini Dar es  Salaam tarehe 28 Julai, 2016.
 Maafisa wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa Mpango Mkakati wa kuhamia Dodoma katika  JIjini Dar es Salaam tarehe 28 Julai,2016 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi hiyo.

Imetolewa na;
Afisa Habari,
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Ofisi ya Waziri Mkuu.
Next Post Previous Post
Bukobawadau