Bukobawadau

MKOA WA KAGERA WAZINDUA RASMI KAMPENI YA HUDUMA JUMUISHI ZA AFYA NA UKIMWI KATIKA WILAYA ZA MISSENYI NA KARAGWE


Mkoa wa Kagera wazindua rasmi Kampeni ya Huduma Jumuishi za Afya na UKIMWI yenye Kaulimbiu “Kuwa Mjanja! Afya ndiyo  dili” katika Halmashauri za Wilaya mbili za Missenyi na Karagwe kwa kulenga kuyafikia makundi mbalimbali ambayo bado hayaweza kupima afya  katika vituo 274 vilivyopo ndani ya mkoa.
Uzinduzi huo wa Kampeni Jumuishi ya Hudunma za Afya na UKIMWI iliyoandaliwa na Shirika la Kimataifa la AMREF HEALTH AFRICA likishirikiana na wadau wengine ambao ni MDH, HUMULIZA na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera pamoja na Hospitali za Wilaya za Missenyi na Karagwe ulifanyika katika uwanja wa Mashujaa Bunazi Wilayani Missenyi.


Akizindua Kampeni hiyo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu aliwashukuru wadau wote walioshirikiana kuandaa kampeni hiyo ili kuweza kuwafikia wananchi walio wengi katika maeneo yao ambao hawajapata wasaa wa kwenda kupima afya zao katika vituo mbalimbali vya afya mkoani Kagera.
“Uzinduzi wa Kampeni hii utasaidia wananchi kupima na kujua afya za wale walioathirika na virusi vya UKIMWI watashauriwa jinsi ya kujitunza na kupewa dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo jambo ambalo litawasaidia wananchi kuyapanga maisha yao mara baada ya kujua afya zao .” Aliststiza Mkuu wa Mkoa Kijuu.
Mhe. Kijuu aliwashauri wananume kutoa ushirikianao kwa wake zao pale wanapohitajika kwenda kupima na kuacha tabioa ya kuamini kuwa wenza wao wakipima tayari na wao wamejua  afya zao jambo ambalo siyo sahihi na ukweli ni kuwa kila mwananchi anatakiwa kujua afya yake yeye mwenyewe.
Akitoa takwimu za Wilaya mbili za Missenyi na Karagwe  Mkuu wa Mkoa Kijuu alisema kuwa kwa kipindi cha Kuanzia mwezi Januari hadi Julai mwaka huu katika wilaya ya Missenyi wananchi waliopima ni 57,459 tu wakati Wilaya hiyo inakadiriwa kuwa na wananchi 202,632  na wananchi 145, 173 bado hawajapima mpaka sasa.


Akitoa takwimu za Wilaya mbili za Missenyi na Karagwe  Mkuu wa Mkoa Kijuu alisema kuwa kwa kipindi cha Kuanzia mwezi Januari hadi Julai mwaka huu katika wilaya ya Missenyi wananchi waliopima ni 57,459 tu wakati Wilaya hiyo inakadiriwa kuwa na wananchi 202,632  na wananchi 145, 173 bado hawajapima mpaka sasa.
Katika Wilaya ya Karagwe wananchi waliopima ni 50,797 kwa kipindi cha Januari hadi Julai 2016 na Wilaya hiyo inakadiriwa kuwa wananchi 332, 020 ambapo wanachi 281,223 hawajapima kujua afya zao katika Wilaya hiyo jambo ambalo sasa wamepata fursa ya kupima afya zao bure bila malipo yoyote.
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa Dk. Thomas Rutachunzibwa alisema kuwa lengo la Kampeni hiyo ni kutoa huduma ya upimaji bure kwa wananchi ili makundi mbalimbali yaweze kufikiwa kwa muda mfupi na kuwahamsisha wananchi kupima kwani walio wengi wanaogopa kupima kwasababu ya gharama za upimaji.
Aidha Dk. Thomas alisema lengo lingine ni kuhakikisha kuwa asilimia 90% ya wananchi katika Wilaya hizo wanapima, wagonjwa ambao wakigundulika kuwa tayari wameathirika  asilimia 90% wapate dawa za kufubaza makaili ya virusi vya UKIMWI pia na kupewa huduma za ushauri nasaha.

Wanaonekana wanafunzi pichani

Katika Halmashauri za Wilaya mbili za Missenyi na Karagwe Kampeni ya huduma Jumuishi za Afya na UKIMWI itafanyika kakika kata 10 kila Halmashauri kwa siku mbili ambapo kwa Missenyi kata hizo ni Buyango, Bwanjai, Kanyigo, Kyaka, Gera, Ishozi, Kashenye, Kasambya, Mutukula na Minziro.
Katika Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe Kampeni hiyo itafanyika katika kata za Kihanga, Kanoni, Kayanga, Bugene, Nyakabanga, Nyaishozi, Kamagambo, Kibondo na Nyakasimbi. “Kuwa Mjanja! Afya ndiyo  dili”

Katika picha ya pamoja


Na Sylvester Raphael
Next Post Previous Post
Bukobawadau