Bukobawadau

HAFLA YA UTILIAJI SAINI MIKATABA 21 KATI YA TANZANIA NA MORROCO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili kwa ajili ya kumpokea Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco leo Ikulu Jijini Dar es Salaam

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na viongozi wa ulinzi wakati wa kumpokea Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco kwa ajili ya hafla utiaji saini wa mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.

Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi wakiwaeleza jambo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli  akiwa na Mgeni wake Mfalme Mohamedi wa Sita wa Morocco mara baada ya kuwasili Ikulu leo Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya hafla utiaji saini wa mikataba 21 kati ya Tanzania na Morocco.