Bukobawadau

TFS WAENDELEA KUTOA MBEGU KWA VIKUNDI MBALIMBALI

NA MWANDISHI WETU
Bukoba.
WAKARA wa huduma za misitu Tanzania (TFS) wanaendelea kutoa mbegu za viriba kwa vikundi mbalimbali na tasisi pamoja na watu binafisi wenye vigezo ili waweze kupanda miti na kurudisha misitu ya asiri ambayo imetoweka.

Hata hivyo Meneja wa (TFS) wilaya Bukoba Braison Paul Mkiwa alisema kuwa ili mtu awenavigezo vya kupewa mbegu hiyo ya seriklai anatakiwa kuwa na shamba lakutosha pamoja na utambulisho wa serikali ya kijiji au kata.
Hata hivyo alisema kuwa mbegu hizo zimetolewa katika maeneo manne mpaka sasa ambapo ni shule ya sekondali Bukara, E.L.C.T Bukoba, Neema group na kwa mtu binafsi Adiventina Kamungi.

Aidha Mkiwa alisema kuwa Serikali kuu kupitia wakala wa huduma za mistu wamekuwa wakitoa mbegu bure kwa wananchi wanaojishughulisha na kilimo cha misitu pamoja na viriba.

Mkiwa alisema katika halmashauri ya Bukoba vijijini zimetolewa mbegu kilo nne na viriba kilo 28 .

Pia alisema kuwa Serikali kwa kujali mahitaji ya wakulima wa misitu ambayo inazinunua mbegu hizo kwa kilo moja shilingi milioni Moja ambapo jumla ya mbegu hizo kilo nne ina thamani ya shilingi milioni nne.
Alisema kuwa viliba vina nunuliwa kwa thamani ya elfu kumi kwa kilo ambayo imegarimu shilingi laki mbili na themanini ambayo imeshatolewa kwa maeneo hayo manne.

Mkiwa alisema kuwa mbengu hizo zimetolewa kilo nne tu ambazo mpaka sasa kwa thamani yake ni shilingi milioni nne tu ikiwa kwa kilo moja inauzwa kwa shilingi milioni moja.

"Wananchi watambue kuwa kilimo hiki cha upandaji miti ni bora sana kuliko watu wanavyo fikiri, na pia wananchi waje wachukue mbegu kwani mbegu zinatolewa bure na serikali hakuna hata senti inayolipwa ili mwananchi apate mbegu"alisema Mkiwa.
Naye mkulima wa misitu Jonasi Mashaka mkazi wa wilaya ya Bihalamuro Kiruruma alisema kuwa kilimo cha misitu ni nibora kama yalivyo mazao mengene hivyo wananchi na jamii kwa ujumla wanatakiwa kuwekeza katika kiliomo hicho.

Mashaka alisema kuwa kilimo cha misitu kinasaidia kuwa na uchumi usio yumba katika familia kwani miti inapo vunwa pale inapo kuwa imekomaa na kuzalisha vitu mblimbali kishelia inasaidia kwa kusomeha watoto na hata kujenga nyumba bora.

"Mimi binafsi nimekuwa nikipanda miti na baadhi ya watu wakinibedha lakini nilipo anaza kuvuna na kuwapeleka watoto wangu katika shule za thamani imekuwa i hudhuni kwa waliokuwa wakiona kuwa napoteza muda tu"alisema Mashaka.

Mashaka aliongeza kuwa jamii itambue kuwa kilimo cha misitu ni cha muda murefu sana lakini pia faida yake ni kubwa mmno tofauti na mazao mengine.
Shirika hilo limedhamilia kurudisha misitu ya asili ambayo imetoweka kutokana na uvunaji ovyo unaotokana na watu wanaohujumu maliasili hiyo kila mara.
Mwisho.
Next Post Previous Post
Bukobawadau