Bukobawadau

KUTOKA KWA MWENYEJI WA MAREHEMU NGWEA UKO SOUTH AFRICA SIKILIZA SABABU ZILIZOPELEKEA KIFO CHAKE

Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia jana.
Hussein Original ambaye yupo Pretoria amesema Ngwear na M to the P ambaye walikuwa room moja wamekutwa wamezima baada ya kuzidhisha madawa ya kulevya...
Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi amefariki akiwa usingizini.

Akiongea na mwandishi wetu muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili za kuamka.

Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka na kuendela na mishemishe yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado hajaamka na ndipo walipogundua kuwa ameshafariki.
Jonathan amesema hakuweza kujua sababu za kifo cha Ngwair kwakuwa maelezo ya daktari yalikuwa kitaalam kiasi cha kushindwa kuelewa. Ngwair alikuwa amepanga kurudi leo nchini.
Next Post Previous Post
Bukobawadau