Bukobawadau

JAMBO BUKOBA YABORESHA SHULE ZA MSINGI WILAYANI NGARA


KAGERA Shirika lisilo la  jambo Bukoba lililoko mkoani Kagera  limetoa msaada wa kujenga baadhi ya miundombinu ya shule tano za msingi  kwenye wilaya kadhaa mkoani humo  kwa lengo la kukuza  vipaji na taaluma kwa wanafunzi wa shule hizo.
Mratibu wa shirika hilo Bw Steven Gonzaga amezitaja shule shule hizo kuwa ni Rulenge (Ngara) matundu manne ya vyoo  , Tumaini (Bukoba Manispaa) madarasa mawili na ofisi ya walimu,  Kalalo (Karagwe) darasa moja  na  Kishoju (Muleba ) iliyotengenezewa madawati 60.
Amezitaja shule nyingine kuwa ni Kasambya (Misenyi) ukarabati wa madarasa mawili na ofisi ya walimu, Kiruruma (Biharamulo) ujenzi wa darasa moja na Karwoshe BK vijijini ukarabati wa madarasa mawili na ofisi ya mwalimu mkuu.
Kwa upande wake afisa elimu wilayani Ngara Simon Mumbee amesema kuwa licha ya jamii kuchangia  miradi kwa kutumia rasilimali zao bado wanahitajika kushirikiana na serikali kupunguza changamoto za miundombinu ya kujifunzia
Mumbee amesema kuwa idara yake kwa kushirikiana na halmashauri ya wilaya hiyo inahamasisha kutenga fedha kwa ajiri ya maboresho ya mazingira ikiwa ni pamoja na kujenga nyumba za walimu na kuweka samani  na vitabu vya kutosha
Hata hivyo Afisa mipango wa halamshauri ya wilaya ya Biharamulo  Zabron Janga kwa niaba ya mkurugenzi wake Nassibu Mbagga  amesema licha ya kupata msaada huo jamii haina budi kuendelea kuchangia  miundombinu  inayokosekana.
“Jamii haina budi  kuchangia miradi ya maendeleo katika kupunguza changamoto za miundombinu katika taasisi za serikali ili kuweza kuboresha maisha ya wananchi wanaohitaji taaluma  ndani na  nje ya nchi”. Alisema Janga
 Aliongeza kuwa jamii inategemea sana kupata misaada na kuzidi kuathiri watoto wao katika kupata taaluma kwenye sekta ya elimu  pamoja na miundombinu mingine katika sekta ya afya  Maji na barabarahuku ikichtumia gharama kubwa kuchangia anasa kwenye sherehe na harusi mbalimbali.
 Afisa Elimu Wilaya ya Ngara Ndg Simon Mumbee akikagua nembo ya Jambo Bukoba.
Pichani  wanafunzi wa shule ya msingi Rulenge wilayani Ngara wakifurahia kujengewa vyoo kwa shilingi milioni 4 na jambo Bukoba ambapo jamii ya shule hiyo imechangia 38% ya ujenzi kwa kukusanya vifaa vinavyopatikana katika mazingira yao
 Afisa Elimu Wilaya ya Ngara Ndg Simon Mumbee katikati katika picha na wa jumbe wa kamati ya shule ya msingi Rulenge
  Afisa Elimu Wilaya ya Ngara Ndg Simon Mumbee akikagua nembo ya Jambo Bukoba.
 Mwalimu Mkuu wa shule ya Rulenge Ndg Mashaka Makemba akitoa  taarifa ya ujenzi na nguvu ya jamii.
  Steven Gonzaga  katika hafla ya kukabidhi Choo cha wanafunzi
 Steven Gonzaga mratibu wa Jambo Bukoba  akikabidhi choo cha kisasa kwa ajili ya wanafunzi wa shule ya Rulenge.
Habari/picha na Shaaban Ndyamukama Ngara
Next Post Previous Post
Bukobawadau