Bukobawadau

MWENGE WA UHURU WATARAJIA KUZINDUA MIRADI YENYE THAMANI YA ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 17.7 MKOANI KAGERA


Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kuzindua miradi ya maendeleo yenye thamani shilingi bilioni 17,729,785,522 Mkoani Kagera ambapo Mwenge huo unatarajiwa kupokelewa Mkoani hapa katikaWilaya Ngara Kata ya Murusagamba mpakani mwa Mkoa wa Kigoma na Kagera tarehe 23/07/2016.
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu  atapokea Mwenge huo kutoka Mkoa wa Kigoma aidha, Mwenge wa Uhuru utakimbizwa Mkoani Kagera katika Halmshauri zote  za Wilaya saba na Manispaa ya Bukoba na kupitia jumla ya miradi 68.
Katika miradi hiyo 68 Mwenge wa Uhuru utazindua miaradi 36, utakagua au kutembelea miradi 17, utaweka mawe ya msingi katika miradi 11, aidha, Mwenge huo utafanya shughuli ya kugawa mizinga na kugawa hundi ili kuhamasisha shughuli za maendeleo katika vikundi kwenye jamii.
Aidha, mchanganuo wa gharama za miradi 68 itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru ni kama ifuatavyo, Serikali Kuu imechangia kiasi cha shilingi 3,811,592,405 sawa asilimia 21.5%. Halmashauri za Wilaya zimechangia kiasi cha shilingi 854,666,220 sawa na asilimia 4.8%
Wananchi wamechangia shilingi 5,507,747,439 sawa na asilimia 31.1% Wahisani wamechangia shilingi 7,555,779,458 sawa na asilimia 42.6% ambapo jumla ya gharama zote kwenye Halmashauri za Wilaya na Manispaa ya Bukoba katika Mkoa wa Kagera ni shilingi 17,729,785,522  sawa na asilimia 100.
Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ni “Vijna ni Nguvukazi ya Taifa Washirikishwe na kuwezeshwa.” Tujenge Jamii Maisha na Utu Wetu; Bila Dawa za Kulevya; Tanzania bila Maambukizi mapya, unyanyapaa na vifo vitokanavyo na UKIMWI; Inawezekana; Timiza wajibu wako kata mnyororo wa rushwa; Wekeza katika Maisha ya baadae; Tokomeza Malaria.
Ujumbe huo unalenga kuwahamasisha wananchi hasa vijana kujikita katika shughuliza uzalishaji badala ya kujihusisha na madawa ya kulevya, uteja, ngono zembe, rushwa pia na kuchukua hatua dhidi ya malaria.
Katika Mkoa wa Kagera Mwenge waUhuru utapokelewa Wilayani Ngara tarehe 23/07/2016 na makabidhiano baada ya Ngara, Karagwe, Kyerwa, Misenyi, Bukoba Vijijini, Manispaa ya Bukoba, Muleba na mwisho ni Wilaya ya Biharamulo na Mkoa utakabidhi Mwenge Mkoa wa Geita.
Next Post Previous Post
Bukobawadau